TAARIFA KWA WAZAZI NA WALEZI
π May 20, 2026 at 6:49 am
πΌ Image
TANGAZO LA MTIHANI WA MOCK KANDA
Wazazi na walezi wote mnapenda kujulishwa kuwa kutakuwa na Mtihani wa Mock Kanda utakaowahusisha wanafunzi kutoka mikoa ya Tabora, Singida, Iringa na Dodoma. Mtihani huo utafanyika tarehe 20.05.2026 hadi 21.05.2026.
Hivyo tunawaomba wazazi muendelee kuwaandaa watoto wenu vizuri kwa kuwapa muda wa kujisomea, kuwahamasisha kufanya marudio ya masomo pamoja na kuhakikisha wanazingatia nidhamu na mahudhurio ya shule katika kipindi hiki muhimu.
Mtihani huu ni hatua muhimu ya kuwaandaa wanafunzi kuelekea mitihani yao ya mwisho na kupima kiwango cha uelewa wao kitaaluma. Ushirikiano wenu ni muhimu sana katika kuwajengea watoto mazingira bora ya kujifunza na kujiamini zaidi.
βTukiwalea watoto katika elimu bora leo, tunajenga taifa imara kesho.β
Asanteni kwa ushirikiano wenu na Mungu awabariki sana.