TANGAZO KWA WAZAZI NA WALEZI
🗓 March 28, 2026 at 7:42 am
🖼 Image
Uongozi wa shule unapenda kuwataarifu wazazi na walezi wote kuwa shule imefungwa rasmi jana tarehe 27/03/2026, na itafunguliwa tena tarehe 08/04/2026 kwa ajili ya kuendelea na masomo ya muhula unaofuata.
Kutokana na mwingiliano wa ratiba ya mitihani ya Darasa la Saba (Pre-Mock na Mock ya Wilaya), tunapenda kuwajulisha kuwa mitihani kwa wanafunzi wa Darasa la Awali hadi Darasa la Sita itafanyika wiki ya pili baada ya kufunguliwa kwa shule.
Aidha, tunapenda kuwajulisha kuwa matokeo ya mtihani wa Mock ya Wilaya kwa Darasa la Saba yatatangazwa hivi punde, na yatapatikana kwenye kipengele cha Mock Wilaya 2026.
Uongozi wa shule unaomba radhi kwa usumbufu wowote ulioweza kujitokeza na tunawashukuru kwa ushirikiano wenu endelevu katika kuboresha elimu ya watoto wetu.
Asanteni kwa ushirikiano