πŸ”– Latest Blog Posts

Showing 10 of 32 posts

AFISA ELIMU MKOA WA TABORA ATOA WITO KWA WAZAZI KUZINGATIA ZOEZI LA UANDIKISHAJI WA WATOTO WA AWALI NA DARASA LA KWANZA KWA MWAKA WA MASOMO 2026.

Afisa Elinu Mkoa wa.Tabora,Mwl Upendo Rweyemamu ametoa rai kwa wazazi na walezi kuhakikisha wanaandikisha watoto wao kwa ajll ya elimu
ya awali na darasa la kwanza mapema kwa ajli ya mwaka wa masomo
2026,ili kutoa nafasi kwa Serikali na wadau wa elimu kufanya maandaliziya
miundombinu na rasilimali muhimu kwa wakati.
Amesema hatua ya uandikishaji wa mapema husaidia kupanga vyema idadi
ya madarasa,walimu na vifaa vya kujifunzia,hivyo kuboresha mazingira ya
ujfunzaji na kuhakikisha kila mtoto anapata haki yake ya msingi ya elimu.
Wakati huohuo,Mwl.Rweyemamu amesisitiza umuhimu wa jamil
kutowaacha nyuma watoto wenye mahitaji maalum,akibainisha kuwa
Serikali imeendelea kuimarisha miundombinu rafiki na kuanzisha shule
maalum na madarasa shirikishi kwa ajlli ya kuwatambua,kuwawezesha na
kuwapatia huduma stahiki za elimu bila ubaguzi.
β€œLakini pia tuna watoto wenye mahitaji maalum ambao wapo kwenye
nyumba zetu,tusiwasahau tumejiandaa kuwapokea,kama unaye mtoto
mwenye mahitaji maalum hakikisha naye pia anaandikishwa,"amesisitiza.

Blog Image Posted on November 27, 2025, 7:59 pm

KIKAO CHA WAZAZI WA WANAFUNZI WANAOSOMA DARASA LA SITA

Tarehe 21/11/2025 mwalimu mkuu amefanya kikao Cha wazazi wa darasa la sita na kueleza mikakati mbalimbali ya kuinua Taaluma na kukuza ufaulu kwa darasa la sita
Katika kikao hicho mwalimu mkuu ameongelea mambo mbalimbali kama ifuayavyo

1.Kuwajali wanafunzi kwa kuwanunulia vifaa vya kujifunzia na sare za shule
2.Kuwafaatilia watoto wao maendeleo ya shule kwa kutumia mfumo wa matokeo unaoitwa mwanzugi.com
3.Kuwa karibu baina ya mzazi na Walimu ili kumuendeleza mwanafunzi

Pia wazazi wamekubaliana kuwa wanafunzi wa Darasa la sita wasifunge shule na wasome kwa wiki tatu wakati wa likizo

Pia Kuwanunulia wanafunzi vifaa vifuatavyo
1.counter book query 3 saba
2.Daftari za msomi saba kwa ajili ya majaribio
3.Kuchangia kiasi cha Tsh. 5,000/= kwa ajili ya mitihani na motisha kwa walimu watakaokuwa wanafundisha wakati wa likizo

Pia mwalimu mkuu amewaomba wazazi kuisemea vizuri shule ya Msingi mwanzugi ili iweze kutangazika vyema

Blog Image

πŸ“Ž Download Attachment

Posted on November 22, 2025, 8:36 pm

KALENDA YA MASOMO MWAKA 2026

*Ufafanuzi wa Kalenda ya Masomo kwa Mwaka 2026 – Tanzania*

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na *Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia*, mwaka wa masomo 2026 kwa shule za awali, msingi na sekondari umegawanyika katika mihula miwili kama ifuatavyo:

*Muhula wa Kwanza (Muhula I):*
- *Unanza:* 13 Januari 2026
- *Likizo fupi:* 27 Machi – 07 Aprili 2026
- *Unafungwa rasmi:* 05 Juni 2026
- *Idadi ya siku za masomo:* 96

*Muhula wa Pili (Muhula II):*
- *Unanza:* 06 Julai 2026
- *Likizo fupi:* 04 – 13 Septemba 2026
- *Unafungwa rasmi:* 04 Desemba 2026
- *Idadi ya siku za masomo:* 98

*Jumla ya Siku za Masomo kwa Mwaka Mzima:*
- *194 siku*

*Maana yake:* Mwaka 2026 kutakuwa na vipindi viwili vya masomo vyenye likizo fupi katikati, na shule zinatarajiwa kufundisha kwa siku 194 jumla. Wazazi, walimu na wanafunzi wanashauriwa kufuata ratiba hii kwa ukamilifu ili kufanikisha malengo ya kitaaluma.

Blog Image Posted on November 21, 2025, 6:26 pm

TANGAZO KWA WAZAZI/WALEZI

Wito wa mkutano mkuu wa Wazazi/Walezi

Blog Image Posted on November 20, 2025, 10:07 am

ZOEZI LA UPIMAJI

Walimu wakitimiza wajibu wao kwa kuwapima wanafunzi uwezo wa kusoma na kurekodi alama zao walizozipata

Posted on November 20, 2025, 8:47 am

MATOKEO YA MTIHANI WA TAIFA DARASA LA SABA 2025

Angalia matokeo ya Mtihani wa Taifa wa darasa la saba 2025 Shule ya Msingi Mwanzugi.
Fungua File hilo hapo chini

πŸ“Ž Download Attachment

Posted on November 11, 2025, 4:05 pm

MTIHANI MWEMA

Mtihani mwema Kidato Cha Pili

Blog Image Posted on November 10, 2025, 7:32 am

MTIHANI WA UPIMAJI KITAIFA DARASA LA NNE

Kila la kheri darasa la nne

Blog Image Posted on October 22, 2025, 5:56 am

TAARIFA KWA WAZAZI NA WALEZI

Habari
Mitihani ya TAMISEMI kwa Darasa la Kwanza na la Pili itaanza Jumatatu tarehe 13/10/2025 hadi Ijumaa 17/10/2025.
Tafadhali mzazi/mlezi hakikisheni watoto wetu wanapata muda wa kupumzika na kujiandaa kikamilifu na zoezi hili la mitihani

Matokeo mtayapata kupitia mfumo wetu wa mwanzugi.com muda wowote baada ya Ijumaa.
Elimu ni msingi wa maisha tusimame pamoja kuwajenga watoto wetu.

Blog Image Posted on October 13, 2025, 10:29 am

MZAZI NA MLEZI

Unakaribishwa kwa heshima kubwa kuhudhuria sherehe ya kuhitimu Darasa la Saba.
Tukio: Sherehe ya Kuaga Darasa la Saba
Tarehe: Jumamosi, 11 Oktoba 2025
Muda: Kuanzia saa 5:00 asubuhi
Mahali: Ukumbi wa St. Joseph
Ni furaha yetu kubwa kushiriki nawe siku hii ya pekee. Tafadhali fika kwa wakati.
Karibu Sana!

Posted on October 9, 2025, 3:12 pm