UJUMBE KWA WAZAZI WA WANAFUNZI WA DARASA LA SABA NA DARASA LA NNE
Wazazi /Walezi,
Tunapenda kukujulisha kuwa bado tunaendelea na mitihani ya maandalizi kwa ajili ya kuwaweka sawa wanafunzi wetu ili wazidi kuwa bora kitaaluma na kifikra.
Utaratibu wa matokeo utakapo tayari:
• Utapokea SMS ya taarifa kwamba matokeo yametoka.
• Fungua Google/Chrome kwenye simu yako.
• Tafuta neno: mwanzugi.com
• Ingia kwenye tovuti kisha chagua “student”.
• Weka (username) na neno siri (password) kuangalia matokeo.
Kumbuka: Utaratibu ni uleule kama ulivyokuwa awali.
🌹 “Mafanikio ya mwanafunzi ni tunda la mshikamano kati ya mzazi, mwalimu na mwanafunzi mwenyewe. Tukisimama pamoja, tutavuna matokeo bora.” 🌹
Posted on August 20, 2025, 6:11 pm
TAARIFA
Tarehe 15/08/2025, siku ya Ijumaa, katika Shule ya Msingi mwanzugi kimefanyika kikao cha tathmini ya kazi za kila idara kwa kipindi cha Julai – Agosti 2025.
Kikao hiki kililenga kupitia mafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizojitokeza pamoja na kuweka mikakati madhubuti ya kuboresha utendaji katika kipindi kijacho. Viongozi wa idara mbalimbali walitoa taarifa zao na mjadala wa pamoja ulifanyika kwa lengo la kuinua kiwango cha taaluma na maendeleo ya shule kwa ujumla.
Kwa pamoja, kikao kiliwahimiza walimu na wafanyakazi wote kuendelea kushirikiana, kuongeza bidii na kuhakikisha shule inaendelea kuwa mfano bora katika elimu na malezi ya mtoto.
Kikao hichi kiliongozwa na:
MWL MKUU: SAID MUNENE
Posted on August 16, 2025, 8:34 am
Habari
Leo tarehe 14.08.2025, shule ya msingi Mwanzugi imefanya kikao cha kitaaluma kwa wazazi wa wanafunzi wa Darasa la Pili, kikiongozwa na Mwalimu Mkuu Said Munene pamoja na walimu wake. Lengo kuu lilikuwa kuwajulisha wazazi maendeleo ya watoto wao kitaaluma na kujadiliana njia bora za kuongeza ufaulu zaidi kwa wanafunzi katika masomo yao pia waweze kufanya vizuri kwenye mtihani wao wa mwisho wa kumaliza darasa la pili.
"Elimu bora ni urithi wa thamani zaidi kwa mtoto."
Kwa mawasiliano zaidi piga simu zifuatazo:
0753576431-MWL MKUU MWANZUGI
0757177828-MWL MKUU MSAIDIZI
0621092667-KATIBU MSAIDIZI WA TAALUMA (MWL WA MIFUMO)
Posted on August 14, 2025, 1:33 pm
Habari mzazi,
Unaombwa kuingia kwenye mfumo wetu wa matokeo ili kuangalia alama za mwanao kwa Testi 1 na Testi 2 za darasa la saba. Tafadhali tembelea mfumo wetu kupitia 'mwanzugi.com' tuliyokupa awali. Asante kwa ushirikiano wako.
Posted on August 14, 2025, 10:05 am