Tarehe 21/11/2025 mwalimu mkuu amefanya kikao Cha wazazi wa darasa la sita na kueleza mikakati mbalimbali ya kuinua Taaluma na kukuza ufaulu kwa darasa la sita
Katika kikao hicho mwalimu mkuu ameongelea mambo mbalimbali kama ifuayavyo
1.Kuwajali wanafunzi kwa kuwanunulia vifaa vya kujifunzia na sare za shule
2.Kuwafaatilia watoto wao maendeleo ya shule kwa kutumia mfumo wa matokeo unaoitwa mwanzugi.com
3.Kuwa karibu baina ya mzazi na Walimu ili kumuendeleza mwanafunzi
Pia wazazi wamekubaliana kuwa wanafunzi wa Darasa la sita wasifunge shule na wasome kwa wiki tatu wakati wa likizo
Pia Kuwanunulia wanafunzi vifaa vifuatavyo
1.counter book query 3 saba
2.Daftari za msomi saba kwa ajili ya majaribio
3.Kuchangia kiasi cha Tsh. 5,000/= kwa ajili ya mitihani na motisha kwa walimu watakaokuwa wanafundisha wakati wa likizo
Pia mwalimu mkuu amewaomba wazazi kuisemea vizuri shule ya Msingi mwanzugi ili iweze kutangazika vyema